Sunday, 24 September 2017

Poetry To Motivate




You cannot change the world, 
But you can present the world with one improved person - Yourself. 

You can go to work on yourself to make yourself
Into the kind of person you admire and respect. 
You can become a role model and set a standard for others. 
You can control and discipline yourself to resist acting
Or speaking in a negative way toward anyone for any reason. 
You can insist upon always doing things the loving way, 
Rather than the hurtful way. 
By doing these things each day, you can continue on your journey
Toward becoming an exceptional human being. 








It is not so much WHERE you live, 
As HOW, and WHY, and WHEN you live, 
That answers in the affirmative, 
Or maybe in the negative, 
The question Are you fit to live?

It is not so much WHERE you live, 
As HOW you live, and whether good 
Flows from you through your neighborhood
. And WHY you live, and whether you 
Aim high and noblest ends pursue, 
And keep Life brimming full and true. 

And WHEN you live, and whether Time 
Is at its nadir or its prime, 
And whether you descend or climb. 
It is not so much WHERE you live, 
As whether while you live you live 
And to the world your highest give, 
And so make answer positive 
That you are truly fit to live. 

Monday, 24 April 2017

CHOMBEZO: ASIA DIGITALI SEHEMU YA KWANZA



CHOMBEZO: ASIA DIGITALI
 

MTUNZI: George Iron Mosenya
 

SEHEMU YA KWANZA.
 

Joto lililokuwa katika chumba kikubwa cha ‘internet café’ liliwafanya wateja wajipepee kwa kutumia makablasha kadhaa waliyoingia nayo ama kuyakuta katika chumba kile.Joto lile lilikuwa kero kwa kila mteja mle ndani, lakini kwa mtu mmoja tu n’do lilikuwa sherehe.Alikuwa ameyaona mawindo sahihi kabisa.Mawindo ambayo yangepewa ushirikiano mkubwa na lile joto.


Mkabala na mahali alipokuwa amekaa alitazamana na kijana wa makamo ambaye afya na mavazi yake pekee yaliidhinisha uwezo wa yeye kuwa ameegesha gari nzuri nje ya jingo lile na mfukoni hakukosa noti kadhaa zenye uzito wa kuitwa pesa. Jasho lilikuwa likimtiririka na alikuwa amejikita katika kujipangusa kwa kutumia leso yake.
 
Kabla umeme haujakatika kijana huyu alifanya siri na kuchungulia mapaja meupe ya binti huyu ambaye hakuteswa na joto lile bali ilikuwa sherehe. Wakati kijana huyu akidhani kuwa alichofanya kilikuwa siri sana…jicho kali na la kitapeli la binti yule liliweza kushuhudia matamanio ya kijana yule.


Sasa umeme ulikuwa umekatika, joto limetawala binti akaamua kuitumia nafasi.
“Atanijua mimi nd’o Asia.” Alijisemea wakati akifungua baadhi ya vishikizo vya blauzi yake. Alifanya hivi huku akkizuga kuwa anateswa sana na lile joto.Maziwa yake ambayo pia yalikuwa meupe pee yalionyesha mchirizi ambao asilimia kubwa ya wanaume wakiutazama hutamani kuona na kinachoendelea chini.


Asia hakuachia uhondo wote, alimuacha yule kijana katika mtihani wa matamanio.Kwa jicho lililofuzu kulaghai wanaume aliweza kuiona suruali ya kitambaa ya yule kijana ikitoka katika kutepeta na kukakamaa.Akafanya tabasamu la kusanifu, akijifanya anaitazama simu yake.Kijana wa watu hakujua kama anachezewa akili.“Kashajileta pumbavu zake.” Aliendelea kufanya tathmini.


Mara akaitupa karata ya mauaji ambayo aliamini kwa namna yoyote lazima yule mwanaume atajiingiza katika himaya yake.Asia kwa kutumia vidole vyake vyenye kucha bandia alibofya simu yake iliyokuwa katika mkoba.Ikaanza kuita akaichomoa. “Hellow……..mwenzangu….yaani najaribu kucheki Bro Smith, Skype umeme nao huko umekatika, nimemcheki kwenye simu, dah network ya Germany sijui vipi. Mbona yamenishuka mwenzako.” Asia aliongea kwa sauti nyororo inayobembeleza na bila shaka ilikuwa inatangaza maisha bora anayoishi kwani alikuwa katika kudeka.
 
Kimya kikatanda kama anayesikilizia kitu fulani kutoka upande wa pili. Kisha akafanya cheko, cheko lililoyaruhusu maziwa yake kifuani kucheza kidogo, akafanya kuiegemea simu akayarekebisha. Jicho lake kama kawaida likamchungulia muhusika wake.
Muhusika alikuwa amesahau kujipepea, alikuwa anatokwa jasho na alikuwa katika kushangaa.“Mi nataka kuondoka hapa, maana hakuna jipya, ..” akaweka kimya tena. Kisha akaendelea.“Naenda Msasani sahivi, lakini shoga mwenzio si unicheke kabisa mapema….sina gari hapa najishaua tu….maza kaenda nalo Mwanza, na mimi kuendesha ka Lexus kake sitaki.”Akaweka nukta tena.


“Mh…atoke wapi wa kunichukua wewe……naenda zangu kupanda daladala mie. Nitafanyaje sasa………baadaye basi Shosti.” Alimaliza maongezi akaufunga mkoba wake baada ya kuwa ameweka simu ndani yake.


Akasimama, akapiga hatua kadhaa, taratibu huku akiruhusu nyamanyama zilizovimbiana kwa nyuma na kumfanya apendeze zikitikisika kwa fujo. Yote haya yalitokea ili fulani aweze kuona.Macho hayana pazia, mikono ikamwenda kinywani, akakunja kunja sharubu zake, kisha mkono mmoja ukamponyoka na kuifikia suruali yake, akauingiza ndani na kusawazisha mambo.Macho ya Asia hayakukosea kumsoma, alikuwa ametamanika.

Kijana akasimama, akajifanya kunung’unika kutokana na huduma mbovu walizopata, hakukumbuka kudai pesa zake.Akapiga hatua kubwa akamfikia Asia.“Vipi dada na wewe wamekuchosha nini? Watu gani hawa yaani umeme umekatika hawawashi jenereta. Aaaargh.” Alilalamika.Asia akajichekesha kisha akasonya.“It’s boring…..yaani dah basi tu….but it sucks….” Akatema maneno, Kiswahili kwa mbali ung’eng’e mwingi.


Wakaendelea na mada ya kuwalalamikia watoa huduma hizo. Hadi wakaufikia ukumbi ule wa kuoneshana nani ni nani.Ilikuwa sehemu ya kuegeshea magari.“Kwani dada unaelekea wapi.” Kijana ambaye alikuwa hajajitambulisha jina akauliza.“Msasani, ngoja nikapate kero nyingine ya kugombania magari. We unaenda pande zipi au safari yetu moja?” aliuliza Asia huku akijua nini kinafuata.


“Mimi nafika Namanga hapo. Kuna watu naenda kuonana nao hivi mara moja. Dah hizi kazi hizi.” Alilalamika katika namna ya kujifagilia njia.“Poa kumbe gari moja twende ukanisaidie kuwania siti.”
 
Jamaa kusikia vile akajikoholesha kisha akamwonyesha Asia kwa kutumia kidole cha shahada, gari aina ya Noah nyeupe ikiwa imetulia ikimsubiri mmiliki. “Mwenzangu heri yako…poa kaka siku nyingine lakini hapa sirudi tena aisee.” Alisema Asia huku akiondoka.“Twende nikusindikize kidogo bwana..” alisihi yule kijana.
 
Asia akajifanya kufikiri kidogo kisha akauliza swali la kijinga.“Hamna mahali unapita maana mimi nina haraka kweli.”“Naenda moja kwa moja.”Asia akakubali, wakaongozana garini.Safari ya kuelekea Msasani.
 
Ndani ya gari maongezi ya hapa na pale yaliendelea….Asia kwa kutumia simu yake akafanya jambo jingine lililompelekea kujikuta anahamishiwa rasmi katika timu nzima ya digitali.Akaandika ujumbe baada ya dakika moja simu yake ikaita.


“Mh…sorry..simu yangu inatatizo la speaker I hope sitakuboa nikitumia loud.” Asia alisema huku akiyafinya macho yake katika namba ya kumhangaisha mwanaume dhaifu. “Aaah…hata usijali ongea tu….” Alijibu.Asia akapokea simu akaiweka katika spika kubwa.“Ehe nambie….” Akaanzisha maongezi. “Peter kanipigia mwenzangu…..”“Anataka nini?”
“Asia jamani…msamehe mwenzako …..kabembeleza sana ujue….” Sauti kutoka upande wa pili ikasihi.”


“Jackline, nakuheshimu sana…nakuomba kwa heshima ya urafiki wetu…usinambie lolote kuhusu huyo tapeli wa mapenzi, Jack umekuwa shahidi wa ujinga alionifanyia Peter….umeshuhudia uchafu wake wote…leo hii unamwombea msamaha…Jack kweli umenichoka kiasi hicho, amekulipa huyo Peter umwombee msamaha……ok Jack labda niseme neno moja tu….ulifurahia alichonifanyia sivyo…..Mbarikiwe sana “ Akamaliza huku analia, akaikata simu, uso ukiwa mwekundu, ngozi yake ya rangi ya chungwa ikikosa ustahimilivu na kuchafuliwa na machozi…kilikuwa kilio haswa. Asia alikuwa analia.


Kijana aliyekuwa anaendesha gari ambaye mwanzoni alikuwa amemtamani Asia alijikuta akipagawa, mara akaiegesha gari pembeni.Vioo vyeusi tii…nani atajua kinachoendelea ndani. Nd’o uzuri wa tinted Akaanza kumbembeleza Asia. Akamsihi sana asilie, Asia akawa analia huku anawalaani wanaume wote. Alimlaani Peter hadi yule kijana naye akamsaidia katika kumlaani.


“Mpendwe vipi nyie wanaume …mnataka roho zetu…mnataka tufe nd’o mjue kuwa mlipendwa au? Yaani mtalaaniwa nasema atalaaniwa huyo Peter, kwa chozi hili linalonitoka mimi Asia…Peter alitaka nini mimi nikamnyima, pesa zangu za kutumia chuo, pesa za kujaza gari mafuta zote nimempa mimi. Alitaka nini sasa, nimepigwa na dadiii mimi mamii akanichukia, kaka zangu wamenipiga makofi mimi. Kisa Peter, Peter….aah…” Asia aliendelea kulaani maneno yaliyomsulubu yule kijana.


Akiwa hajui cha kufanya Asia akiwa analia alimlalia, alimlalia kifuani, zile chuchu alizoziona kwa kuibia kule ‘internet café’ sasa zilikuwa zimemlalia zikimchoma katika namna ya kuleta hamasa, kucha za bandia za Asia zikalifinyafinya shingo lenye afya la yule kijana.


Pumzi za kupishana ndani na nje zikawa zinatesa katika sikio la yule kijana. Sasa alianza kupagawa. Huyu Asia alikuwa anajibembeleza ama.Akawa katika sintofahamu. Nani atampa jibu?Asia akalisikia paja lake likiguswa na kitu ambacho hakikuwepo hapo awali. Hakushtuka Akafanya tabasamu jepesi kisha akamzomea yule jamaa.Hicho kitu kilivimba kutoka katika suruali nyepesi.


“Bwege linawahi kweli kupata hamu hili.” Asia alikebehi kimya kimya.Hamu zikamzidi yule kijana, mara naye akakumbatia, mara akakumbatia kwa nguvu zaidi. Mara akaanza kunena katika lugha za maajabu zisizojulikana kitaifa wala kimataifa.


Mikono yake ilikuwa ikitalii katika mzigo wa titi mbili ndogo za Asia.Afadhali yeye alikuwa ananena kilugha.Asia alikuwa hoi kama aliyezirai.Jamaa akajua kuwa Asia kakolea.Laiti kama angejua kuwa Asia anatumia mbinu ya kidigitali, basi ni heri angebaki katika dunia ya analojia aliyokuwa anaishi awali.


“Baby…..Baby…..unaniua mweenzio….unaniaaa…..pliiz stop…..” “Am sore bebi…am sore vere sore….me you know…” Jamaa akajaribu kiingereza asichokijua, Asia akataka kupitiwa na kicheko.Akajikaza. Alikuwa kazini.


Mkono wa jamaa ukapenya katika mapaja…..Asia akajua jamaa anataka kumpima kina cha kisima na kutazama kama kina maji ama ni kikavu.“Bwege asije akanichafua bure..akavuka mipaka…..”Asia digitali akacheza kidigitali, alishagundua kuwa jamaa ni mwepesi sana.


Ulimi mkali kama ule wa kinyonga, ulimi ambao ulishausema uongo hadi uongo ukauzoea ukazama katika sikio la yule jamaa.“Uwiiiiiii….ooooohhh yeees..” jamaa akaganda kama roboti, mkono haukwenda mbele wala kurudi nyuma.Akazidi kunena kwa lugha zake zisizokuwa za kiroho.Asia akagundua kuwa amefanikiwa kwa kiasi kikubwa.Akafanya tekniki ya mwisho.Akajibandua katika mwili wa jamaa….akaanza kujifuta midomo, na kujifanya anaona aibu……jamaa kaduwaa tu hajui digitali inakwenda vipi. Analojia ilikuwa imemwathiri.
 
Jamaa akawa na aibu za kweli, suruali ilikuwa wima sana. Akajitazama, shughuli ikaja je airekebishe ama aicha ilivyo………

****Huyu ndiye Asia Digitali…….je historia yake inaanzia wapi…ni lini alihamia digitali…chanzo cha kuaicha analojia ni kipi???

****NI MWANZO TU WA CHOMBEZO HILI LA AINA YAKE AMBALO LINAKUWEKA KATIKA HALI MBILI, KICHEKO NA HISIA……..KAZI NI KWAKO…. ENDELEA KUTEMBELEA

Uteuzi wa Jokate Mwegelo UVCCM Waibua Mfarakano

Uteuzi  wa Miss Tanzania namba mbili wa mwaka 2006, Jokate Mwegelo kuwa Kaimu Katibu wa Uhamasishaji wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, unaonekana kutaka kuivuruga jumuiya hiyo.

Mjadala mkubwa umeibuka kuhusu uteuzi huo, ambapo baadhi ya wanachama na viongozi wa juu wa jumuiya hiyo wamedai kuwa haukufuata kanuni na taratibu za umoja huo.

Vyanzo vya kuaminika kutoka katika umoja huo vimedai kuwa baadhi ya viongozi wa juu wa UVCCM hawakushirikishwa katika uteuzi huo uliofanywa na kigogo mmoja wa umoja huo.

Taarifa za ndani zinaeleza kuwa uteuzi huo haukushirikisha wajumbe wa Kamati ya Utekelezaji wala Baraza Kuu la UVCCM, ambalo halikukutana kumthibitisha Jokate kama kanuni zinavyoelekeza.

Kwa mujibu wa kanuni za jumuiya hiyo, wajumbe wa kamati ya utekelezaji hawazidi 10, ambapo miongoni mwao ni Mwenyekiti wa umoja huo Taifa, Makamu Mwenyekiti Taifa, Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu na mjumbe mmoja kutoka makao makuu ya chama.

Wajumbe wa baraza kuu ni wenyeviti na makatibu wa mikoa na mjumbe mmoja kutoka katika kila mkoa.

Kutokana na kile kilichodaiwa kuwa ni mvurugano ndani ya umoja huo, Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa, Shaka Hamdu Shaka, amesema kuwa uteuzi huo ulifuata taratibu zote za chama.

“Ni kweli amekaimishwa kwa kufuata taratibu zote za chama, kikao cha Kamati ya Utekelezaji kilikutana Aprili 18, mwaka huu, Dar es Salaam na ndicho kimewakaimisha wakuu wa idara watano akiwamo Jokate.

“Hao wanaolalamika hawajui kanuni na taratibu za jumuiya yetu, huwezi kupata nafasi kama kikao cha Kamati ya Utekelezaji hakijakaa,” alisema Shaka.

Hata hivyo alikiri kutoitishwa kwa kikao cha Baraza Kuu ili kuthibitisha uteuzi huo, akisema ni gharama kubwa kuitisha kikao hicho.

“Kwa kawaida Baraza Kuu huwa linakutana kila baada ya mwaka mmoja, kuita baraza kuu ni gharama sana hivyo ikitokea kuna nafasi wazi Kamati ya Utekelezaji ina mamlaka pia ya kumthibitisha,” alisema.

Kwa upande wake, Jokate alishukuru kwa uteuzi huo na kuahidi kuifanya jumuiya hiyo iwe karibu zaidi na vijana wa Kitanzania.

“Nashukuru kwa imani waliyoonyesha viongozi wangu ila zaidi kuona nina uwezo wa kuongoza idara hiyo nyeti na muhimu kwenye jumuiya.

“Kikubwa ni kuifanya jumuiya iwe karibu zaidi na vijana wa Kitanzania na kurudisha tumaini na kusimamia changamoto wanazozikabili vijana katika kujiletea maendeleo,” alisema Jokate.

Jokate pia alikuwa miongozi mwa wanachama 450 wa CCM waliojitokeza kuchukua fomu za kuwania ubunge wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA).

Jokate alianzia kwenye mashindano ya Miss Tanzania mwaka 2006 ambapo aliibuka mshindi wa pili.

Hivi sasa anajishughulisha na sanaa na ujasiriamali ambapo anamiliki Lebo ya Kidoti Fashion inayojihusisha na uuzaji wa nywele na mavazi.

Poetry To Motivate

You cannot  change  the world,  But you can present the world with one improved person - Yourself.  You can go to work on yourself to m...